LIVERPOOL FC YAMNASA KIPA LORIS KARIUS KWA MKATABA WA MUDA MREFU
Mchaka mchaka wa usajili umeanza kupamba moto!!!Klabu ya Liverpool imetangaza rasmi kukamilika kwa usajili wa mlinda mlango Loris Karius kutoka klabu ya FSV Mainz 05 mwenye umri wa miaka 22 kwa mkataba wa muda mrefu mara baada ya kufuzu vipimo vya afya klabuni hapo.
Akizungumza na mtandao wa timu hiyo Karius alisema "Ni hisia nzuri sana na ni heshima kuichezea klabu kama hii.
Kipa huyo amethibitishiwa kuvaa jezi namba moja ambayo hapo awali ilikuwa ikivaliwa na Brad Jones pamoja na wakongwe David James, Jerzey Dudek pamoja na Sander Westerveld.
Karius anakuwa mchezaji mpya wa pili kuwasili Liverpool hadi sasa baada ya Joel Matip kusajiliwa mapema mwaka huu na na alihitaji hitimisho la mkataba wake wa sasa na FC Schalke.
-Liverpoolfc.comKarius atajumuishwa rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai MosiKarius atajumuishwa rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai MosiKarius atajumuishwa rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai Mosi
0 comments:
Post a Comment