Tuesday 24 May 2016

LIVERPOOL FC YAMNASA KIPA LORIS KARIUS KWA MKATABA WA MUDA MREFU






Mchaka mchaka wa usajili umeanza kupamba moto!!!Klabu ya Liverpool imetangaza rasmi kukamilika kwa usajili wa mlinda mlango Loris Karius  kutoka  klabu ya FSV Mainz 05 mwenye umri wa miaka 22 kwa mkataba wa muda mrefu mara baada ya kufuzu vipimo vya afya klabuni hapo.



Akizungumza na mtandao wa timu hiyo Karius alisema "Ni hisia nzuri sana na ni heshima kuichezea klabu kama hii.

Loris Karius

Kipa huyo amethibitishiwa kuvaa jezi namba moja ambayo hapo awali ilikuwa ikivaliwa na Brad Jones pamoja na wakongwe David James, Jerzey Dudek pamoja na Sander Westerveld.

Karius ambaye ameiwakilisha  Ujerumani katika ngazi ya U21 , alicheza mechi  34 za Bundesliga msimu uliopita , ambapo  hakuruhusu goli katika mechi tisa na kusaidia Mainz kumaliza ligi katika nafasi ya sita atajumuishwa  rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai Mosi.

Karius anakuwa mchezaji mpya wa pili kuwasili Liverpool hadi sasa baada ya  Joel Matip kusajiliwa mapema mwaka huu na na alihitaji hitimisho la mkataba wake wa sasa na FC Schalke. 
-Liverpoolfc.com
Karius atajumuishwa  rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai Mosi
Karius atajumuishwa  rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai Mosi
Karius atajumuishwa  rasmi katika kikosi cha Liverpool Julai Mosi

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA