NI MIUJIZA TU KWA MANCHESTER UNITED KUNUSA TOP FOUR MSIMU HUU
Kipa mahiri wa Manchester United akijaribu kuuzuia bila mafanikio mpira ulioipa Westham goli la ushindi |
MANCHESTER United sasa inasubiri miujiza kumaliza katika
nafasi ya nne katika Ligi Kuu ya England baada ya kukubali kichapo cha bao 3-2.
Kabla ya mchezo wa huo wa kiporo uliochezwa Jumanne usiku kwenye dimba la Upton
Park, United ilikuwa na matumaini ya kumaliza
katika nafasi ya tatu, lakini sasa imebakiwa na nafasi finyu ya kushika nafasi
ya nne.
Mfungaji wa bao la ushindi Winston Reid akiwaongoza wenzake kushangilia mara baada ya kupachika goli la tatu |
United yenye pointi 63 sasa italazimika kushinda mchezo wake wa mwisho
dhidi ya AFC Bournemouth Mei 15 halafu iombe Manchester City yenye pointi 65
ifungwe na Swansea City, kinyume na hapo, klabu hiyo ya Old Trafford itajikuta
ikiambulia nafasi ya kucheza Europa League msimu ujao huku Champins League
ikiota mbawa kwao.
West Ham ilikuwa ya kwanza kufunga katika dakika ya 10
kupitia kwa Diafra Sakho bao lililodumu hadi mapumziko. Anthony Martial akaifungia
United mabao mawili katika dakika ya 58 na 72 na kuifanya West Ham ikicharuke
na kupata magoli yaliyokuja dakika ya 76 na 81 yaliyofungwa na Michail Antonio
na Winston Reid.
MSIMAMO WA LIGI BAADA YA MECHI HII
0 comments:
Post a Comment