MWANAMUZIKI CHRISTINA GRIMMIE AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI KICHWANI
Mwanamuziki Christina Grimmie ambaye aliwahi kushiriki katika kipindi cha televisheni cha The Voice, amepigwa risasi kichwani na kufa baada ya kumalizika tamasha lililofanyika Orlando, polisi wa Florida wamesema.
Taarifa imeeleza kuwa Grimmie alipigwa risasi na mshambuliaji huyo wakati akitia saini yake kwa moja wa shabiki, ambapo mshambuliaji huyo alidhibitiwa na kaka wa Grimmie lakini baadaye alijipiga risasi na kujiua.
Grimmie mwenye umri wa miaka 22, alifariki dunia baadaye akiwa hospitali. Mwaka 2014 Grimmie alifanikiwa kumaliza shindano la kuimba la The Voice na kushika nafasi ya tatu.
0 comments:
Post a Comment