Sunday 17 July 2016

HUKUMU::ASKARI ALIYEMUUA MWANAHABARI MWANGOSI AFUNGWA JELA MIAKA 15



Mjane wa marehemu Daudi Mwangosi akizungumza na wanahabari ikiwa ni pamoja na kuwashukuru kwa umoja wao . 

Rais wa umoja wa klabu za waandishi wa habari Tanzania Bw Deo Nsokolo akizungumza na wanahabari baada ya hukumu ya kesi ya mauwaji ya Mwangosi 
Na MatukiodaimaBlog , Iringa 
MAHAKAMA kuu kanda ya Tanzania kanda ya Iringa imemhukumu kwenda jela miaka 15 askari Polisi Kikosi cha Kutuliza Ghasia ( FFU )Iringa namba G 58 Pacificius Cleophace Simon (27) kwa kosa la kumuua bila kukusudia mwaahabari Daudi Mwangosi mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi. wakati akiwa katika majukumu yake ya kuchukua habari huku mke wa marehemu Mwangosi Itika Mwangosi akipongeza vyombo vya habari nchini kwa ushirikiano mkubwa katika kufuatilia kesi hiyo. 

"Mahakama inatambua uchungu wa familia iliyoupata kwa kifo cha marehemu Daudi Mwangosi ambaye aliuwawa pia marehemu aliuwawa kikatili ....siku zote adhabu inapaswa kulingana na kosa husika mahakama haiafiki maombi ya wakili wa upande wa utetezi kuomba mshtakiwa apewe adhabu ya kuachiwa huru kwa kuwa ni yatima ....mgongano wa hisia umeonekana katika kesi hii ila mahakama inampa adhabu ya kwenda jela miaka 15" alisema jaji Dkt Paul Kiwelo.

Akisoma shauri ya kesi hiyo kabla ya kutoa adhabu leo mahakamani hapo jaji Dkt Kiwelo aliwashukuru wazee wa baraza la mahakama kwa michango yao mkubwa mchango ulioisaidia mahakama hadi kufikia siku hiyo ya hukumu pia mawakili wote walioshiriki katika kesi hiyo.

" Suala la aina gani ya adhabu inafaa halikuwa rahisi sana kwani shauri hili upande wa jamhuri uliomba adhabu ya kufungwa maisha jela huku upande wa utetezi ukiomba mshitakiwa aachiwe huru kwa masharti ambayo mahakama ingeona yanafaa kutokana na kuwa na majukumu ya kulea wadogo zake na yeye kuwa yatima .....mahakama imetazama ukubwa wa kosa husika pia jamii ina mtazamo gani katika kesi hiyo lakini mahakama haitoi hukumu kwa mitazamo mbali mbali inatumia vifungu vya sheria suala la kutoa adhabu ni la kisheria si vinginevyo".

Jaji Dkt Kiwelo alisema kuwa adhabu haitolewi kwa ajili ya kulipiza kisasi ila inatolewa kama sehemu ya onyo na kuifanya jamii kutambua kuishi kwa kuheshimu misingi ya sheria kwani kuna mambo manne katika kesi yanatazamwa likiwemo la medhania ya kosa alilotenda na aina ya kosa pia maslahi ya jamii katika kosa husika.

Wanahabari mkoa wa Iringa wakimsikiliza Bw Nsokolo leo 

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA