Thursday, 11 August 2016

ATABAKI:::LEICESTER CITY YATANGAZA KUMBAKIZA MAHREZ KIKOSINI


Leicester City inaamini kuwa Riyad Mahrez ataendelea kuitumikia timu hiyo katika msimu mpya unaoanza wikiendi hii kufuatia mazungumzo ya kina na mkurugenzi wa klabu hiyo Jon Rudkin. Arsenal imekuwa ikihusishwa kwa karibu na usajili wa Mahrez lakini mabingwa hao wa England hawana dhamira ya kumuuza nyota huyo wa kimataifa wa Algeria mwenye umri wa miaka 25. Kiwango cha Mahrez kimemkuna  Arsene Wenger lakini kocha wa Leicester Claudio Ranieri ameendelea kusisitiza kuwa nyota huyo haondoki.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA