KUFUZU UEFA::SERGIO AGUERO APIGA HAT-TRICK ,MAN CITY IKISHINDA 5:0
Sergio Aguero amefunga magoli matatu yaani hat-trick wakati Manchester City ikiichakaza magoli 5-0 Steaua Bucharest katika mchezo wa kwanza wa kuwania kufuza Ligi ya Mabingwa.
Aguero pia alikosa penati mbili katika mchezo huo, ya kwanza iliokolewa na kipa na ya pili alipaisha mpira, huku David Silva akifunga goli la kwanza katika dakika ya 13.
Sergio Aguero alifunga goli lake la kwanza na kufanya matokeo kuwa 2-0 na kuongeza mengine mawili baada mchezaji mpya wa Manchester City Nolito kufunga goli la tatu.
Sergio Aguero akikosa moja ya penati mbili alizochemsha
Mshambuliaji Nolito akiifungia Manchester City goli la tatu
Sterling alikuwa katika kiwango bora na kusaidia kupatikana kwa magoli mawili
0 comments:
Post a Comment