Wednesday 14 December 2016

SERIKALI YATANGAZA AJIRA KWA WALIMU WA MASOMO YA HISABATI NA SAYANSI

SERIKALI imetangaza kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika shule za sekondari ambao wametakiwa kupeleka nakala za vyeti vyao vya elimu ya sekondari, vya taaluma ya ualimu (stashahada na shahada) kwa ajili ya uhakiki.

Tangazo kwa Umma lililotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish lilisema vyeti vya sekondari vinavyotakiwa kuhakikiwa ni vya kidato cha sita.

Alisema ajira hizo ni kwa walimu wa Stashahada na Shahada za Mafunzo ya Ualimu wa Masomo ya Hisabati na Sayansi waliohitimu mwaka 2015.

Alisema nakala hizo ziwasilishwe kupitia barua pepe ya wizara kuanzia jana hadi Ijumaa ya Desemba 16 mwaka huu na yeyote ambaye vyeti vyake havitahakikiwa hatafikiriwa katika uajiri.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA