Monday 9 January 2017

LIONEL MESSI AIOKOA BARCELONA NA KIPIGO DHIDI YA VILAREAL

Lionel Messi ameiokoa Barcelona isipate kichapo kupitia mkwaju wa adhabu wa dakika za mwisho na kuinyima Villarreal ushindi katika mchezo wa La Liga jana.

Nicola Sansone aliwapatia wenyeji goli la kuongoza kwa shuti la chini akipokea pasi ya mchezaji wa zamani wa Chelsea, Alexandre Pato.

Katika mchezo huo shuti la Messi liligonga mwamba na Barcelona walinyimwa penati pale Bruno aliposhika mpira wa shuti la Messi.

Kwa matokeo hayo ya goli 1-1 Barcelona inabakia katika nafasi ya tatu, ikiwa nyuma ya vinara Real Madrid kwa tofauti ya pointi tano.
                       Lionel Messi akipiga mpira wa adhabu katika dakika ya 90 na kuzaa goli
                                Kiungo Sergio Basquets akimfanyia madhambi Alexandre Pato

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA