KOMBE LA FA : LIVERPOOL YABANWA NA PLYMOUTH
Kikosi cha vijana wa Liverpool kimejikuta kikidhibitiwa na kutoa sare tasa na timu ya daraja la pili ya Plymouth Argyle katika mchezo wa raundi ya tatu wa kombe la FA katika dimba la Anfield hii leo.
Wenyeji Liverpool ambao wachezaji wake walikuwa na wastani wa miaka 21, walimiliki mpira kwa asilimia 80.3 katika kipindi cha kwanza huku Sheyi Ojo akishindwa kutumia nafasi nzuri kufunga.
Katika mchezo huo Divock Origi pia goli lake lilikataliwa kutokana na kumchezea rafu Gary Miller, kabla ya kocha Jurgen Klopp kuamua kuingiza kikosi cha kwanza cha kawaida cha kina Daniel Sturridge, Adam Lallana na Roberto Firmino.
Mpira uliopigwa na Sheyi Ojo ukidakwa na kipa
Jitihada za Divock Origi zikigonga ukuta wa timu ya Plymouth
0 comments:
Post a Comment