Monday 16 May 2022

PROF. MBARAWA ASISITIZA UMUHIMU WA WATALAAM WA UJENZI KUJENGEWA UWEZO

 

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, akisisitiza jambo katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi lililofanyika mkoani Tabora.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt. Batilda Burian, akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), (hawapo pichani) katika mkutano wao ulioanyika mkoani Tabora.
Naibu Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Bw. Ludovick Nduhiye, akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, mkoani Tabora. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Burian na Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bw. Eric Lengama.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Burian, Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Balozi, Eng. Aisha Amour, pamoja na viongozi wengine wa Baraza la Wafanyakazi wakiimba wimbo wa mshikamano katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Balozi, Eng. Aisha Amour, akizungumza mbele ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa, ambaye ni mgeni rasmi mara baada ya kufungua kikao cha Baraza la Wafanayakazi lililofanyika mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Balozi, Eng. Aisha Amour, akiteta jambo na Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta hiyo, Bw. Fanuel Muhoza, katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, mkoani Tabora.
Katibu wa TUGHE Tawi la Sekta ya Ujenzi, Bw. Mussa Sillas, akiongoza wimbo wa mshikamano (Solidarity Forever), kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, mkoani Tabora.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani), mkoani Tabora.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani), mkoani Tabora.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani), mkoani Tabora.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesisitiza umuhimu wa watumishi wa (Sekta ya Ujenzi), kujengewa uwezo na ujuzi katika utekelezaji na usimamizi wa miradi inayoendelea ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Prof. Mbarawa amesema hayo mjini Tabora, wakati akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Sekta hiyo ambapo pamoja na mambo mengine amesisitiza umuhimu wa wataalam wa usanifu wa barabara, madaraja na majengo kujiimarisha na kupata uzoefu ili kuboresha utendaji kazi na kupunguza gharama zinazoongezeka katika miradi kutokana na kukosewa kwa usanifu.

“Hakikisheni mnawapa ujuzi wa kutosha watalaamu wote ili waweze kuwa wabunifu, wanaojiamini na wenye uwezo mkubwa wa kusimamia miradi”, amesema Prof. Mbarawa.
Katika hatua nyingine, Waziri Prof. Mbarawa ameitaka Wizara pamoja na Wakala wa Barabara (TANROADS), kusimamia kwa karibu malalamiko katika vituo vya mizani ili kuhakikisha mizani zote nchini zinakuwa katika ubora wakati wote na kutoa huduma nzuri kwa wadau wa usafirishaji.

Amesisitiza umuhimu wa watumishi wa Sekta ya ujenzi kufanya mazoezi kila wakati ili kujiepusha na maradhi yasiyoambukizwa na hivyo kuwa na rasilimali watu kubwa yenye afya njema katika utekelezaji wa miradi.
Naye, Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo Balozi Eng. Aisha Amour, amemhakikisha Waziri Prof. Mbarawa kuwa watumishi wa Sekta hiyo wamejipanga kuhakikisha wanasimamia miradi yote ya ujenzi iliyopitishwa kwenye Bajeti kikamilifu na hivyo kufikia malengo yaliyopangwa na Wizara.

Balozi Aisha amesema wamejipanga kutoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa wataalam ili kuwajengea uwezo wa kuendana na mabadiliko ya mara kwa mara ya teknolojia na hivyo kuleta tija na ufanisi mahali pa kazi.

Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi Sekta ya Ujenzi pamoja na mambo mengine umepitisha rasimu ya bajeti ya Sekta hiyo kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA