Showing posts with label vunja mbavu. Show all posts
Showing posts with label vunja mbavu. Show all posts

Friday, 23 September 2016

Sunday, 10 July 2016

HAPANA CHEZEA KIFO:::FISI AJIFICHA NDANI YA MZOGA KUYAOKOA MAISHA YAKE

Habari Mdau wa Funguka Live ,leo nimeona tujikumbushe kisa hiki cha kusisimua sana ambapo ni nadra sana kupatikana , nimatumaini yangu utafurahi na kujifunza kitu.
 Na  Stratton Hatfield

Katika kujiokoa kwenye hatari yeyote ile si tu watu ambao wanaweza kupata wazo la ajabu la kutenda ilimradi tu kuepukana na mauti, fisi mmoja aliyekuwa katika lishe yake alijikuta katika wakati mgumu baada ya kulazimika kujificha kwenye tumbo la mzogo wa tembo ili kumkwepa simba dume aliyemvamia ghafla.

Fisi huyo aliyaona mauti yaleeeeee, lakini aliona ni heri kukaa ndani ya tumbo la tembo kulikoni kuliwa na simba. picha zifuatazo zinaonyesha namna fisi huyo alivyojificha na baadae kufanikiwa kukimbia baada ya kupata upenyo.

Tukio hilo halijatokea mbali bali ni kule Masai Mara, pata uhondo huo.


Simba akiwa katika doria kumsubiri mtuhumiwa wake ambaye naye aliendelea kujichimbia mafichoni humo
Taswira ya fisi ndani ya mzoga
  

Hali ilipokuwa shwari alichomoka kwa mwendo kasi
Simba akiendelea kumfukuza mtuhumiwa wake hata baada ya kuchomoka mafichono


Photo Credit ::Hatfield & Klaassen

    Friday, 24 June 2016

    AMKODISHA MPENZI WAKE ILI APATE PESA YA KUNUNUA I PHONE 6


    Mwanafunzi wa Chuo kikuu kimoja cha China ambaye jina lake halikutambulika kwa haraka ameamua kufanya ‘uchizi’ ili mradi tu aipate pesa ya kununua aina mpya ya iPhone iliyoingia sokoni, iPhone6. Kijana huyo wa alionekana akiwa nje ya chuo kikuu cha Songijiang akiwa na bango kubwa lililoandikwa kwa kichina na kutafsiriwa ‘Girlfriend Sharing’.


     Katika tangazo hilo kijana huyo anaeleza kuwa yuko tayari kumkodisha mpenzi wake kwa mtu yeyote atakayeweza kutoa pesa ili jamaa apate kiasi cha kutosha kuinunua iPhone 6 yenye screen kubwa. Picha ya kijana huyo imesambaa kwa kasi katika mtandao wa kijamii unaotumiwa na wachina uitwao ‘Weibo’ ambao ni kama Twitter. Tangazo hilo limeambatana na picha za mpenzi wake na amewatoa hofu wateja wanaosita kuingia nae mkataba kuwa hata mpenzi wake ameridhia na yuko tayari kudate na mtu yeyote atakaejitokeza.Muda wa kuwa na msichana huyo baada ya kumkodi umebainishwa kutokana na malipo yatakayofanywa na mteja. 

    Viwango ni vya saa 1 (10 yuan), siku 1 (50 yuan) au mwezi mmoja (500 yuan). Hata hivyo, wapenzi hawa sio wa kwanza kujiweka sokoni ili wapate bidhaa ya kampuni ya Apple. Mwaka jana katika uzinduzi wa iPhone 5, wanandoa wa Shaghai waliwaweka sokoni watoto wao watatu ili wapate pesa ya kununua computer na simu za iphones lakini walikamatwa na kufunguliwa mashitaka. 

    Lakini pia kijana mdogo wa Hunan alijitolea kuuza figo lake ili apate pesa ya kununua iPad na iPhone. Siyo hayo tu, hivi karibuni mwanaume mmoja wa Saudi Arabia ametaka kupewa iPhone 6 kama mahari ya dada yake hata kabla aina hiyo ya simu haijazinduliwa Bahrain

    Monday, 6 June 2016

    MUHITIMU WA CHUO AVUA NGUO JUKWAANI ALIPOITWA KUPEWA CHETI



    \


    Wasomi wanapokutana hasa katika zoezi la kutunukiwa cheti kama kielezo cha uhitimu wa ngazi fulani kuna vitu huwezi kuvifikiria kama vitatokea hata kidogo.
    Katika Jack Britt High School, North Carolina, Marekani wanafunzi mmoja amewaacha hoi mamia ya watu waliohudhuria sherehe ya kutunukiwa vyeti (graduation) baada ya kupanda jukwaani kupokea cheti chake na ghafla akavua johon lake na kubaki na boxer.



    Baada ya kuvua joho alinyoosha mikono yote miwili juu kama mwanamieleka anayetamba. Lakini haikuchukua round wanausalama wakamdhibiti na kumuweka chini ya ulinzi.


    Kwa mujibu wa The Huffington Post, kijana huyo alinyang’anywa diploma yake na hivyo hakukabithiwa cheti.


    Hata hivyo bado anahesabiwa kama mtu aliye maliza masomo yake na kuhitimu licha ya kuwa hana kielelezo cha elimu yake.
    “Shule yetu imefanya jitihada kubwa.

    Hapo zamani watu waliohudhuria walikuwa wenye vurugu wakati wa graduation. Tumefanya jitihanda kuwafanya watu waheshimu wanafunzi.

    Huyu kijana amechagua kutoonesha heshima kwa wanafunzi wenzake.” Alisema Dr Frank Till, mwalimu wa chuo hicho.

    Tuesday, 21 April 2015

    PACHA WA FELLAINI NI SOO!! ACHANGANYA WATU MOURINHO KIDOGO NAE ACHANGANYWE> CHEKI HAPA

    Sikia hii kali, Kocha Jose Mourinho aliambiwa kiungo mrefu wa Man United, Marouane Fellaini hatacheza mechi dhidi ya Chelsea.



    Kisa, mfungua mlango wa hoteli alimueleza Mourinho kwa Fellaini alikwenda kuchukua tiketi za kuingia katika mechi hiyo kwa mmoja wa wachezaji wa Chelsea.

    Kumbe, mfungua mlango huyo wa hoteli alijichanganya kwa kuwa mtu huyo alikuwa ni pacha wa Fellaini aitwaye Mansour.

    Baadaye Mourinho akaingia kuingia kwenye mtandao na kugundua yule mhudumu wa alijichanganya.
    -SALEHE JEMBE

    Thursday, 19 March 2015

    MAJAJI WATATU WAFUKUZWA KAZI BAADA YA KUKUTWA WAKIANGALIA FILAMU ZA NGONO KWENYE KOMPYUTA ZA MAHAKAMA

    Majaji watatu wamefutwa kazi kwa kutumia muda wao afisini kutizama filamu za ngono.
    Jaji Timothy Bowles anayesikiza kesi za wilaya , jaji wa maswala ya uhamiaji Warren Grant na jaji Peter Bullock wamefutwa kazi.
    Majaji hao walipatikana na hatia ya kutumia mtandao rasmi wa mahakama kwa mujibu wa wachunguzi wa idara ya mahakama.
    Maafisa hao wanasemekana kuwa walitazama mitandao yenye filamu za ngono huku wakifahamu vyema kuwa ilikuwa ni ukiukaji wa sheria za matumizi kwa mujibu wa msimamizi wa idara hiyo ya Mahakama.
    >>BOFYA HAPA KUDOWNLOAD ANDROID APPLICATIO YA FUNGUKA LIVE BLOG ILI HABARI ZIKUFIKIE MOJA KWA MOJA KATIKA SIMU YAKO<<
    Hata hivyo kiongozi wa idara ya mahakama hiyo ya Uingereza na jaji mkuu waliwapata na hatia ya kwenda kinyume cha maadili ya mahakama.
    Jaji wa nne Andrew Maw aliamua kustaafu mwenyewe wakati uchunguzi huo ukiendelea badala ya kufikishwa kizimbani.
    Mwandishi wa BBC wa maswala ya kisheria Clive Coleman kuwa makosa hayo yalikuwa makubwa sana katika mizani ya uadilifu wa majaji.
    Aidha hakuna hata mmoja wao atakayeruhusiwa kufanya kazi katika idara ya mahakama tena.

    Saturday, 7 February 2015

    KALI YA MWAKA BIBI WA MIAKA 94 AKAMATWA AKISAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA KWA STYLE YAKIPEKEE....CHEKI PICHA

    Sina hakika hii imetokea nchi ipi  Japo inaashiria ni kama mashariki ya Kati.
    Inasemekana amehukumiwa kifungo cha siku 12 jela na kama ataendelea atakuwa hai basi kifungo kitaongezwa.
    Kama hukumu hii ni ya kweli Basi itakuwa iliyovunja rekodi.....
    VIA WHATSAP

    Monday, 26 January 2015

    Kutana na Jamaa aliyewauzia watu Mkojo Wa Binadamu Akiwadanganya ni Ni Pombe Kali!







    Jamaa mmoja amefikishwa mahakamani Uingereza, kitendo alichokifanya wengi hawakupendezwa nacho!

    Nicholas Stewart alitumia chupa zenye nembo ya Smirnoff, Jack Daniels pamoja na Vodkaili watu wasigundue kwamba anachowauzia haikuwa whisky, chupa hizo zilijazwa mkojo.
    Mshtakiwa huyo alikamatwa siku ya pili baada ya kuwauzia wateja kwa wingi mkojo huo aliokuwa amechanganya na maji ambapo alikua akitumia kipimo kile kile ambacho hutumika kupimia whisky.

    Mwendesha mashtaka Victoria Cartmell kabla ya kutoa hukumu alipokea majibu kutoka kwa mkemia Mkuu ambapo yalionyesha kwamba kilichokuwa kwenye chupa sio whisky feki ila ilikuwa ni mkojo, adhabu aliyopewa haikuwa kifungo cha jela kama ambavyo wengi walitarajia, amefungiwa kufanya biashara ya kuuza vinywaji kwa miezi 2.

    Sunday, 28 December 2014

    OFFICIAL MEMBER

    OFFICIAL MEMBER

    Please Share This Site

    HABARI ZETU

    LIKE PAGE YETU HAPA