Sunday 23 March 2014

CHELSEA YAIBANDUA ARSENAL

Wachezaji wa Chelsea wakishangilia baada ya kuifunga Arsenal bao la tano leo kwenye Uwanja wa Stamford Bridge jijini London .
Mchezaji wa Arsenal Kieran Gibbs (kushoto) akipewa kadi nyekundu kipindi cha kwanza.
CHELSEA imeifanya kitu kibaya Arsenal baada ya kuichapa mabao 6-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya England ‘Premiership’, leo kwenye Uwanja wa Stamford Bridge jijini London.
Arsenal ambayo iliingia uwanjani katika mechi ya 1,000 tangu kocha wa timu hiyo, Arsene Wenger alipoanza kuinoa timu hiyo, imekutana na kipigo hicho lakini kukatokea tukio la kushangaza la kadi nyekundu.
Mabao ya Chelsea kwenye mchezo huo yamepatikana kupitia kwa Samuel Eto'o dakika ya 5, Andre Schürrle (7), Eden Hazard (17), Oscar (42 na 66) na Mohamed Salah (71).

Tukio la kushangaza ni kuwa mwamuzi alimpa kadi nyekundu Gibbs wa Arsenal wakati aliyetenda kosa la kuunawa mpira kwa makusudi ni Oxlade-Chamberlain katika dakika ya 15.


Chelsea Line-up: 1Petr Cech, 2Branislav Ivanovic, 24Gary Cahill, 26John Terry, 28César Azpilicueta, 4David Luiz, 11Oscar,14Andre Schürrle, 17Eden Hazard, 21Nemanja Matic,29Samuel Eto'o Substitutes: 23Mark Schwarzer, 33Tomas Kalas, 8Frank Lampard, 12John Mikel Obi, 15Mohamed Salah, 9Fernando Torres, 19 Demba Ba

Arsenal Line- up: 1Wojciech Szczesny, 3Bacary Sagna, 4Per Mertesacker, 6Laurent Koscielny, 28 Kieran Gibbs, 7Tomas Rosicky, 8 Mikel Arteta, 9 Lukas Podolski, 5 Thomas Vermaelen, 15 Alex Oxlade-Chamberlain, 19 Santi Cazorla, 12 Olivier Giroud

Substitutes: 21Lukasz Fabianski, 5Thomas Vermaelen, 25Carl Jenkinson, 20Mathieu Flamini, 29Kim Kallstrom, 22Yaya Sanogo,44Serge Gnab
ry

 Kiufupi jana timu vigogo zilijizolea mabao mengi  pale Liverpool walipoilaza Cardif goli 6 -3 ,huku Manchester city wakiibugiza Fulham 5 bila katika michezo hii Suarez wa Liverpool na Yahya Toure wa Mancity walipiga hatrik. 
kwa matokeo haya nafasi ya ubingwa msimu huu bado ni kitendawili kwani Chelsea (kinara) inapointi 69 mechi ilizocheza ni 31 huku Liverpool (nafasi ya pili) ikiwa na pointi 65 akicheza mechi 30 nae Manchester  city (nafasi ya tatu) ikiwa na pointi 64 ikicheza michezo 27.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA