Saturday 29 March 2014

KASHFA YA USHOGA YAMTESA ASHLEY COLE..AKUNUSHA


MAPEMA wiki iliyopita uvumi ulisambaa nchini England kwamba gazeti maarufu la The Sun lilikuwa mbioni kuchapisha stori ndefu iliyohusu kashfa ya ushoga ya mlinzi mmoja wa sasa wa kushoto wa timu ya taifa ya England.
Hata hivyo, Gazeti la The Sun la juzi Jumapili lilikanusha kutaka kuandika stori hiyo, lakini bado mlinzi wa kushoto wa England na Chelsea, Ashley Cole akawahi kukanusha kwamba alikuwa hahusiki na kashfa hiyo.
Cole ameimiliki nafasi ya ulinzi upande wa kushoto tangu Machi 2001 na ndiye mchezaji wa pembeni aliyecheza mechi nyingi zaidi katika kikosi cha timu ya taifa ya England.
Na kama kutakuwa na ukwlei wowote katika habari hiyo ni wazi kwamba hilo litakuwa pigo jingine kwa mchezaji huyo ambaye kwa sasa anahaha kupata namba hiyo hiyo aliyoitawala muda mrefu katika kikosi cha Chelsea na hivyo hiyo kuwa nuksi nyingine inayomuandama mchezaji huyo.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA