Tuesday 3 June 2014

Sakata la Mbasha: Kanisa la Ufufuo na Uzima Latoa Tamko Lake Kuhusu Tukio Hilo




Ni wiki sasa pamekuwa na gumzo hapa jijini juu ya tuhuma Za Ubakaji zinazomkabili mume wa mwimbaji mashuhuri Flora Mbasha. Na Kwa Makusudi na yamkini kikundi flani cha watu wamehusisha sakata hili na Kanisa letu la Ufufuo na Uzima, tena Kwa maneno makali sana. Bahati mbaya watu hawa wamewakosesha baadhi ya watanzania wasiojua Chochote na kujikuta nao pia wamo kwenye kumbo la kutukana, kumkashifu na wakati mwingine kutukana viongozi wa Dini kitu ambacho ni kibaya kinawaletea laana Binafsi. Kwa mustakabali huo ni Vema Basi waziwazi tukaongea sintofaham hii na kujibu maswali ya kila mwana jamii juu yetu. Siku zote Ufufuo na Uzima tumekuwa mbele kutolea ufafanuzi kila sentensi inayolenga huduma hii na kanisa la Mungu kwa ujumla wake hapa Tanzania.

Ifahamike tu wazi kwamba sakata hili tunalisikia sana mitandaoni. Kanisa kama kanisa hatujui lolote wala Chochote juu ya sakata hili, lilianza wapi linakwenda wapi na litafikia wapi. Ni Kweli Flora Mbasha na Mumewe mara Nyingi hupenda kushiriki nasi Kwenye ibaada zetu. 

Kanisa limejikita zaidi na huduma ya kiroho. Hatumaanishi kwamba washirika wetu hawapati mitatizo ya kiutu au kijamii, tunaamini Msingi Wetu hasa ni Maombi. Na Kama kukiwa Na tatizo la kijamii viko vyombo husika vya serikali yetu ambavyo ni wajibu wao kutekeleza majukumu Yao. 


0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA