Friday 11 December 2015

LIVERPOOL YAFUZU "32 BORA" EUROPA,YAUNGANA NA MACHESTER UNITED



Liverpool's Belgian forward Divock Origi (right) stretches to take the ball down during the final Group B clash 

TIMU ya Liverpool imewafuata mahasimu, Manchester United katika 32 Bora ya michuano ya UEFA Europa League baada ya kulazimisha sare ya 0-0 ugenini jana na FC Sion katika mchezo wa mwisho wa Kundi B wa michuano hiyo Uwanja wa Tourbillon. Liverpool sasa inamaliza kileleni mwa kundi hilo, baada ya kutimiza pointi 10, mbele ya FC Sion iliyomaliza na pointi tisa. Mchezo mwingine wa kundi hilo, Bordeaux imelazimishwa sare ya 2-2 na Rubin Kazan Uwanja wa Matmut Atlantique, hivyo kupoteza nafasi ya kusonga mbele.
Despite the frozen conditions on ground, James Milner (right) of Liverpool makes a crunching tackle on Sion's Ebenezer Assifuah Ikumbukwe Manchester United imeangukia katika Europa League baada ya kutolea katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa ya UEFA.
Sasa timu hizo zitasubiri droo itakayochezeshwa siku ya jumatatu ili kujua nani anamkabili nani katika hatua ya 32 bora.

 

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA