TUZO YA ATE YAPOKELEWA KWA FURAHA NA WAFANYAKAZI WA TBL
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Dar es Salaam katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
Ofisa
Mipango wa Kampuni ya TBL Group kutoka Dar es Salaam, Tumaini Moses
akiwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Songwe mkoani Mbeya akiwa na Kombe
la tuzo ya Mwajiri bora 2015 ambayo kampuni hiyo ilishinda hivi
karibuni.Hafla yakupokea kombe ilifanyika mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wa Mbeya katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wa Mwanza katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
Baadhi
ya wafanyakazi wa TBL Mwanza katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya
kushangilia ushindi iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Dar es Salaam katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
Wafanyakazi
wa kampuni ya Tanzania Breweries Limited Group katika mikoa ya Dar
es Salaam,Mwanza,Mbeya na Arusha wameshiriki kusherehekea mafanikio ya
kampuni yao kwa kuibuka mshindi wa tuzo ya mwajiri bora kwa mwaka 2015
ambayo ilitunukiwa hivi karibuni na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE).
Ushindi
huu umekuwa shirikishi kwa wafanyakazi wote ambapo kombe la tuzo hiyo
limetembezwa katika viwanda vya kampuni vilivyopo katika mikoa
mbalimbali ambapo wafanyakazi walilipokea na kufanya hafla za
kusherehekea ushindi huo.
Mkurugenzi
wa Raslimali Watu wa TBL Group David Magese alisema kuwa ushindi huu na
mafanikio mengine ya kampuni hayahusu uongozi pekee bali wafanyakazi
wote wa kampuni “ushirikishwaji wa wafanyakazi wote katika mafanikio
yetu ni jambo ambalo tunalizingatia sana na ndio maana tumeamua
kulizungusha kombe hili la tuzo ya mwajiri bora kwao ili washerehekee
ushindi huu kwa kuwa ni miongoni mwa wadau wakubwa wa mafanikio
haya”.Alisema.
Magese
aliongeza kusema kuwa TBL Group ambayo pia inashikilia tuzo ya Mlipa
Kodi bora nchini mbali na ushindi huu wa jumla mwaka huu pia ilishinda
tuzo zingine tofauti ambazo ni Uzingatiaji Kanuni Bora za
Uongozi,Uongozi na Utawala,Uzingatiaji wa Kanuni za Raslimali Watu
,Ubora na Uzalishaji,Kujari na kuthamini walemavu na tuzo ya Taasisi
Bora inayoongoza kwa Ukubwa.
“Mwaka
jana kampuni ya TBL ilishinda tuzo ya jumla katika kipengele cha
Mahusiano mazuri na wafanyakazi ambayo inadhihirisha kuwa kampuni
imeweka mazingira bora ya kufanyia kazi na inawajali wafanyakazi wake
katika ngazi zote.Tuzo hiyo pia ilitambua kuwa TBL imejenga mazingira
bora na uongozi makini unaozingatia vigezo bora vya ajira na kujenga
mazingira mazuri ya kazi kwa waajiriwa wake”.
Alimalizia
kwa kusema kuwa kampuni hiyo inao wafanyakazi 2,100 nchini kote wakiwa
wanafanya kazi za ufundi,Mauzo na Usambazaji,na katika vitengo
mbalimbali vya biashara na kati ya hao wapo wenye ajira za kudumu na
ajira za muda na kuongeza kuwa itaendelea kutoa motisha kwa
wafanyakazi,kujali afya zao na kuzingatia zaidi kanuni za usalama kazini
pia kuwaendeleza wafanyakazi wake kimafunzo ili kuongeza ufanisi zaidi.
0 comments:
Post a Comment