dar 3
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Dar es Salaam katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
mbeya 1
Ofisa Mipango wa Kampuni ya TBL Group kutoka  Dar es Salaam, Tumaini Moses akiwasili kwenye Uwanja wa  ndege wa  Songwe mkoani Mbeya akiwa na Kombe la tuzo ya Mwajiri  bora 2015 ambayo kampuni hiyo ilishinda hivi karibuni.Hafla  yakupokea kombe ilifanyika mwishoni mwa wiki.
mbeya 7
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wa Mbeya katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
mwanza  5
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL wa Mwanza katika picha ya pamoja wameshikilia  kombe la ushindi.
mwanza 2
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Mwanza katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya kushangilia ushindi iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
TBL ATE 1
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Dar es Salaam katika picha ya pamoja wameshikilia kombe la ushindi.
Wafanyakazi wa kampuni  ya Tanzania Breweries Limited  Group  katika mikoa ya Dar es Salaam,Mwanza,Mbeya na Arusha wameshiriki kusherehekea mafanikio ya kampuni yao kwa kuibuka  mshindi wa tuzo  ya mwajiri bora kwa mwaka 2015 ambayo ilitunukiwa hivi karibuni na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE).
Ushindi huu umekuwa shirikishi kwa wafanyakazi wote ambapo kombe la tuzo hiyo limetembezwa katika viwanda vya kampuni vilivyopo katika mikoa mbalimbali ambapo wafanyakazi walilipokea na kufanya hafla za kusherehekea ushindi huo.
Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL Group David Magese alisema kuwa ushindi huu na mafanikio mengine ya kampuni hayahusu uongozi pekee bali wafanyakazi wote wa kampuni “ushirikishwaji wa  wafanyakazi wote katika mafanikio yetu ni jambo ambalo tunalizingatia sana na ndio maana tumeamua kulizungusha kombe hili la tuzo ya mwajiri bora kwao ili washerehekee ushindi huu kwa kuwa ni miongoni mwa wadau wakubwa wa mafanikio haya”.Alisema.
Magese aliongeza kusema kuwa TBL Group ambayo  pia inashikilia tuzo ya Mlipa Kodi bora nchini mbali na ushindi huu wa jumla mwaka huu pia ilishinda tuzo zingine tofauti ambazo ni Uzingatiaji Kanuni Bora za Uongozi,Uongozi na Utawala,Uzingatiaji wa Kanuni za Raslimali Watu ,Ubora na Uzalishaji,Kujari na kuthamini walemavu na tuzo ya Taasisi Bora inayoongoza kwa Ukubwa.
“Mwaka jana kampuni ya TBL ilishinda tuzo ya jumla katika kipengele cha Mahusiano mazuri na wafanyakazi ambayo inadhihirisha kuwa kampuni imeweka mazingira bora ya kufanyia kazi na inawajali wafanyakazi wake katika ngazi zote.Tuzo hiyo pia ilitambua kuwa TBL imejenga mazingira bora na uongozi makini unaozingatia vigezo bora vya ajira na kujenga mazingira mazuri ya kazi kwa waajiriwa wake”.
Alimalizia kwa kusema kuwa kampuni hiyo inao wafanyakazi 2,100 nchini kote wakiwa wanafanya kazi za ufundi,Mauzo na Usambazaji,na katika vitengo mbalimbali vya biashara na kati ya hao wapo wenye ajira za kudumu na ajira za muda na kuongeza kuwa itaendelea kutoa motisha kwa wafanyakazi,kujali afya zao na kuzingatia zaidi kanuni za usalama kazini pia kuwaendeleza wafanyakazi wake kimafunzo ili kuongeza ufanisi zaidi.