UHOLANZI YAILAZA UINGEREZA NYUMBANI KATIKA DIMBA LA WEMBLEY
Timu ya Uingereza iliyojaa matumaini baada ya ushindi dhidi ya Ujerumani imejikuta ikifungwa mabao 2-1 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Uholanzi ambayo haikufuzu michuano ya Euro 2016.
Katika mechi hiyo ya jana usiku iliyopigwa kwenye dimba la Wembley timu hizo zilisimama kucheza katika dakika ya 14 ili kutoa heshima kwa mchezaji wa zamani nyota Johan Cruffy aliyefariki dunia.
Janssen akifunga goli la penati na kumpoteza kipa Fraser Forster
Jamie Vardy akifurahi bao alilofunga akiwa na Kyle Walker
0 comments:
Post a Comment