BARCELONA YAZIDI KUANDAMWA NA JINAMIZI LA VIPIGOA LA LIGA
Lionel Messi amefikisha magoli 500 tangu aanze kucheza soka, baada ya kufunga goli moja jana lakini halikutosha kuisaidia Barcelona kupata ushindi baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Valencia.
Kwa kipigo hicho Barcelona inaweka rekodi mbaya ya kufungwa mara tatu mfululizo katika Ligi ya Hispania La Liga, ikiwa ni mara ya kwanza kupata kichapo cha mfululizo cha namna hiyo tangu mwaka 2003.
Goli la mpira uliogongwa na Ivan Rakitic uliotokana na krosi ya Guilherme Siqueira uliingia wavuni na kujifunga kabla ya baadaye Santi Mina kumalizia shambulizi hatari na kuandika bao la pili kwa Valencia katika kipindi cha kwanza.
Ivan Rakitic akimfunga kipa wake kimakosa
MSN wakiwa hawaamini matokeo
0 comments:
Post a Comment