Friday 13 May 2016

EVERTON YAMFUNGASHIA VIRAGO KOCHA ROBERTO MARTINEZ

Image result for ROBERTO MARTINEZ

ROBERTO MARTINEZ ametupiwa virago na Everton, uamuzi ulioripotiwa kuchukuliwa kufutia timu yake kuchapwa mabao 3-0 na Sunderland Jumatano, matokeo ambayo yamewathibitishia wapinzani wao hao kubaki Premier League. 

Image result for ROBERTO MARTINEZEverton ambayo kwa sasa inakamata nafasi ya 12 katika ligi, imefanikiwa kushinda mara moja tu katika mechi kumi za mwisho za Premier league.
 Kocha huyo Mhispania alitua Goodison Park mwaka 2013, akitokea kufanya kazi Swansea City na Wigan Athletic. Ni kocha wanne kufundisha muda mrefu katika Premier League kati ya makocha wa sasa baada ya Arsene Wenger, Eddie Howe na Mark Hughes.


 Martinez mwenye miaka 42, ametimuliwa huku akiwa bado na miaka mitatu katika mkataba wake aliosaini kiangazi cha mwaka 2014.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA