MAJERUHI :: WELBECK KUIKOSA MICHUANO YA EURO
DANNY Welbeck atakosa fainali za Euro 2016 baada ya vipimo
vya awali kuonyesha kuwa huenda akawa nje ya uwanja kwa miezi mitano. Straika
huyo wa Arsenal alipata majeraha ya goti wakati wa ipindi cha kwanza cha mechi
yao ya Jumapili waliyotoka sare ya 2-2 dhidi ya Manchester City baada ya
kugongana na Bacary Sagna.
Welbeck alifahamu haraka kwamba tatizo hilo ni kubwa
kutokana na uzoefu alioupata katika majeraha mengine tofauti ya goti
yaliyomuweka nje ya uwanja kwa miezi 10. Vipimo vya awali vimeonyesha kuwa
straika hyo, 25, atakosa kuitumikia timu ya taifa ya England katika Euro 2016
na huenda akakosekana pia katika mwanzo wa msimu ujao wa Arsenal.
Nyota huyo wa
zamani wa Manchester United alifunga magoli matano na kutoa “asisti” mbili wakati
waliporejea bada ya kusubiriwa sana Februari na kuwa mchezaji muhimu katika
kikosi cha Arsenal Wenger katika siku za mwisho za msimu.
Uthibitisho wa ukubwa
wa tatizo ulitarajiwa kutolewa jana, lakini vipimo vya awali vinaonyesha kwamba
Welbeck, pamoja na majeruhi Alex Oxlade Chamberlain, hawatashiriki fainali hizo
za mataifa ya Ulaya nchini Ufaransa Juni, mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment