JESHI LA MISRI LATOA PICHA ZA MABAKI YA NDEGE YA EGYPTAIR
Jeshi la Misri limetoa picha za vitu vilivyopatikana katika zoezi la kuitafuta ndege ya shirika la EgyptAir iliyotoweka katika eneo la bahari ya Mediterranea.
Picha hizo zinaonyesha vitu kama jaketi la kujiokolea, sehemu za viti na vitu vingine mbalimbali vinavyoonyesha ni vya ndege hiyo aina ia Airbus.
Ndege hiyo ilitoweka Alhamisi ikiwa angani ikitokea Jijini Paris kwenda Cairo ikiwa na abiria 66 pamoja na wahudumu.
Jaketi la kujiokolea maisha mtu akiwa majini la ndege hiyo
Sehemu ya mabaki ya viti vya ndege kama inavyoonekana kwenye picha hii
0 comments:
Post a Comment