Sunday, 14 August 2016

MOURINHO AANZA KWA USHINDI,ZLATAN AKIFUNGUA AKAUNTI YA MABAO

Zlatan Ibrahimovic amefunga goli katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uingereza wakati Manchester United ikiibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Bournemouth na kumpatia kocha wao mpya Jose Morinho ushindi wa kwanza.

Katika mchezo huo Juan Mata alikuwa wa kwanza kuifungia Manchester United katika dakika ya 40 kufuatia makosa yaliyofanywa na mabeki wa Bournemouth, ambapo baadaye katika dakika ya 59 Wayne Rooney alifunga la pili kwa mpira wa kichwa.

Zlatan Ibrahimovic alijitambulisha rasmi katika Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kufunga goli la tatu kwa shuti la mbali mnamo dakika 64 lililomshinda golikipa, kisha Adam Smith akaifungi Bournemouth goli pekee katika dakika ya 69.
    Juan Mata akifunga goli la kwanza la Manchester United baada ya mabeki kufanya uzembe
   Zlatan Ibrahimovic akiangalia shuti lake aliloachia likielekea wavuni na kuandika goli la tatu
   Mchezaji mpya wa Manchester United Eric Bailly ambaye ametajwa kuwa mchezaji bora katika mchezo huo, akituliza mpira gambani huku akiwa ameruka juu

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA