Wednesday 30 November 2016

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOANI ARUSHA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MHE. Kassim Majaliwa  anatarajiwa kutembelea Jiji la Arusha kuanzia kesho tarehe 01 hadi 03/12/2016 na kukagua miradi ya maendeleo, kuongea na watumishi wa Jiji, kukutana na wafanyabiashara pamoja na kuzungumza na wananchi.

Kwa mujibu wa Afisa habari wa Jiji la Arusha Nteghenjwa Hosseah, kesho tarehe 01/12/2016 Waziri mkuu MHE. KASSIMU MAJALIWA atatembelea National Milling Company (NMC) na pia atakagua ujenzi wa barabara ya Friends Corner - Muriet yenye urefu wa Km 7 inayojengwa kwa kiwango cha Lami kupitia mradi wa Mpango Mji Mkakati (TSCP) na kusimamiwa na Ofisi ya Rais Tamisemi.

Hosseah amesema siku ya tarehe 02/12/2016 Waziri Mkuu atakutana na kuzungumza na watumishi pamoja walimu katika Ukumbi wa AICC Arusha na baadae atakutana na wafanyabiashara katika Ukumbi huo.

"Katika siku ya tatu ya ziara yake Mhe Majaliwa  atatembelea na kukagua viwanda vya Lodhia pamoja na Hans Paul vilivyoko mtaa wa Viwanda – Njiro na baadae atakutana na wanachi wote kwenye Mkutano wa hadahara utakaofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid kuanzia saa nane mchana."

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA