Thursday 26 January 2017

SOUTHAMPTON YAFUZU FAINALI KOMBE LA EFL KWA KUIFUNGA LIVERPOOL


Southampton imeitoa Liverpool katika michuano ya kombe la EFL na kutinga nusu fainali ya michuano hiyo kwa kuifunga goli 1-0, na kuifanya kuibuka na ushindi wa jumla ya magoli 2-0.



Southampton walishuka katika mchezo huo wakiwa tayari wanaongoza kwa goli moja la mchezo wa awali lililofungwa na Nathan Redmond katika dimba la St Mary.




Katika mchezo huo Daniel Sturridge alikosa nafasi mbili za kufunga na kupaisha mpira juu huku Fraser Forster akifanikiwa kuokoa mpira uliopigwa Emre Can.



Goli la Southampton lilifungwa na Shane Long baada ya kufanyika shambulizi la kasi katika dakika za mwisho.

                                  Mshambuliaji Daniel Sturridge akipaisha juu mpira na kukosa goli 
        Kipa Fraser Forster akifanya kazi ya ziada kuokoa mpira uliopigwa na Emre Can 

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA