Sunday 23 January 2022

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA KUENDELEZA USHIRIKIANO UJENZI WA MIUNDOMBINU NCHINI



Waziri wa ujenzi na uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amekutana na Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB), Bw, Amos Cheptoo na kumhakikishia kuwa Tanzania itasimamia kikamilifu utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu yote inayopata fedha toka benki hiyo kwa kuzingatia thamani  ya fedha.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Waziri Prof Mbarawa amesema mazungumzo hayo yataongeza kasi ya utoaji fedha kutoka katika bank hiyo hasa kwa miradi ya viwanja vya Ndege ambayo imechelewa kutokana na changamoto mbalimbali. 

Ameitaja baadhi ya miradi inayoendelea kujengwa kupitia fedha za AfDB ni pamoja na barabara na viwanja vya ndege katika mikoa mbalimbali nchini.

"Tumejipanga kuunganisha mikoa yote ya Tanzania  na maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa mazao kwa barabara za lami ill kukuza uchumu",amesema Prof. Mbarawa.

Mkurugenzi mtendaji huyo wa AfDB Bw, Cheptoo amesema benki hiyo  itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha adhma ya ujenzi wa miundombinu ya kisasa hususan barabara na viwanja vya ndege inatekelezeka.

Baadhi ya miradi hiyo ni barabara za Kabingo-Kasulu-Manyovu km 260.6 km mkoani Kigoma, Mnivata-Newala-Masasi km 160 mkoani Mtwara na uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA