Thursday, 22 May 2014

Gharama za maisha zapaa Samunge


Maelfu ya vijana kutoka sehemu mbalimbali nchini wapo Samunge kuchimba dhahabu katika Mto uliokauka wa Karabaline huku wakisema wanapata dhahabu yenye ubora wa juu kuliko ya mahali pengine.PICHA|MAKTABA 
Na Mwandishi Wetu, Mwananchi

Posted  Alhamisi,Mei22  2014  saa 24:0 AM
Kwa ufupi
Ndoo ya maji Sh2,000 sahani ya wali Sh6,000, Babu aomba msaada wa Serikali


Maelfu ya vijana kutoka sehemu mbalimbali nchini wapo Samunge kuchimba dhahabu katika Mto uliokauka wa Karabaline huku wakisema wanapata dhahabu yenye ubora wa juu kuliko ya mahali pengine.
Baadhi ya wachimbaji kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Morogoro na Msumbiji, walisema dhahabu inayopatikana katika mto huo ambao umevamiwa kwa zaidi ya kilomita nne, inaelezwa imesambaa hadi katika mashamba na milima ya Kijiji cha Mgogo, Samunge.
Mchimbaji Mashaka Kasunga alisema dhahabu ya hapo haipatikani maeneo mengine nchini.
Alisema yeye na wenzake 30 wenyeji wa Ushirombo, Shinyanga ndiyo walikuwa wa kwanza kuchimba madini hayo Aprili mwaka huu baada ya kupata taarifa ya kuwapo kwake.
“Tulikuwa Singida machimboni ikaletwa dhahabu iliyotolewa mlimani hapa tukaiona ni bora sana ndipo tukaja tukachimba awamu ya kwanza na kupata gramu 116 na tukaenda kuuza,” alisema.
Mchimbaji John Kefa alisema hajui walipata gramu kiasi gani lakini wachimbaji wengine walipata kilo moja ya dhahabu ambayo waliuza zaidi ya Sh50 milioni.
Mchimbaji mzoefu, Sophita Malembeka alisema mashamba mengi yanayopakana na Mto na Mlima Mgongo yana dhahabu, hivyo kuomba waruhusiwe kuchimba pia kuupasua mlima.
Wachimbaji wengi walisema kwa siku zinapatikana gramu kati ya 100 na 200 za dhahabu ambazo katika eneo hilo zinauzwa hadi Sh60,000 kwa gramu.
Mchimbaji mwingine, David Selea alisema kwa wastani kama wakiwa na maji ya kutosha katika eneo la mita tano wamekuwa wakipata kati ya gramu tatu hadi tano kwa siku.
Mnunuzi wa madini, Charles Malongo kutoka Bariadi, Simiyu alisema kwa siku hununua hadi gramu 100 na dhahabu ya eneo hilo ni bora kwa asilimia 99.
NA MWANACHI

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA