Thursday 31 December 2015

AZAM YAREJEA KILELENI LIGU KUU BARA

Azam FC imezidi kupambana kwenda kileleni baada ya kuitwanga Mtibwa Sugar kwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.

Bao pekee la Azam FC lilifungwa na nahodha wake, John Bocco katika dakika ya 86 kwa mkwaju wa penalti.

Hata hivyo, Mtibwa Sugar watajilaumu wenyewe kwa kupoteza nafasi nyingi zaidi za kufunga.

Ushindi huo unaifanya Azam FC kufikisha pointi 35 na kuendelea kubaki katika nafasi ya pili nyuma ya Yanga.


Mtibwa Sugar inaendelea kubaki katika nafasi ya tatu ikiwa  na pointi 27.
-Picha na Bin Zubery

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA