Tuesday 19 April 2016

RAIS MAGUFULI KULIZINDUA DARAJA LA KIGAMBONI LEO


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo jumanne ( 19/04/2016 ) anatarajiwa kulizundua daraja la kisasa la Kigamboni.

Daraja hilo la kisasa kabisa lenye urefu wa mita 680 ni kiunganishi muhimu kwa eneo la Kigamboni na Kurasini wilayani Temeke jijini Dar es Salaam.

Kuzinduliwa kwa daraja hilo kutapunguza msongamano wa magari na abiria ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakitumia vivuko kuingia na kutoka Kigamboni.

Wadau mbalimbali wameupongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, NSSF kwa kusimamia mradi huo hadi kukamilika kwake.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA