TIMU YA VIJANA CHELSEA WATWAA TENA UBINGWA WA UEFA
Wakati wakubwa zao wakifanya vibaya, timu ya vijana ya Chelsea imefanikiwa kutwaa kwa mara ya pili mfululizo taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa Vijana baada ya kuwafunga wenzao wa PSG kwa mabao 2-1.
Beki wa Chelsea Fikayo Tomori aliipatia timu yake goli la kuongoza katika dakika 10. Baada ya kukosa penati katika kipindi cha kwanza PSG ilisawazishwa kupitia kwa Yakou Meite, hata hivyo baadaye Casey Palmer aliifungia Chelsea goli la pili.
Vijana wa Chelsea wakiwa na kombe pamoja na medali zao
Casey Palmer akishangilia na wenzake goli la pili alilofunga
0 comments:
Post a Comment