Thursday 7 April 2016

WOLFSBURG YAIDUWAZA REAL MADRID KWA KIPIGO CHA 2-0


Timu ya Wolfsburg imeiduwaza Real Madrid kwa kupata ushindi rahisi wa mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya uliopigwa Ujerumani.

Wenyeji walizawadiwa penati ya utata wakati Casemiro alipoonekana kama amemfanyia mazambi Andre Schurrle, na Ricardo Rodriguez kupachika bao kwa mkwaju wa penati.

Real Madrid ambao walikuwa dhaifu upande wa beki, walijikuta Bruno Henrique akimtengenezea pande Max Arnold na kufunga bao la pili.
   Ricardo Rodriguez akimpoteza mahesabu kipa wa Real kwa mkwaju wa penati na kuandika bao
                                      Max Arnold akishangilia baada ya kufunga bao la pili
                                         Tabasamu la uchungu wa kukosa nafasi ya kufunga 

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA