BAYERN WAMUAGA PEP GUARDIOLA KWA MVUA YA POMBE
Baada ya misimu mitatu, Pep Guardiola ameiaga Bayern Munich
kwa shangwe za aina yake baada ya mchezo wa mwisho wa Bundesliga ulioisha kwa
ushindi wa 3-0 dhidi ya Hannover.
Guardiola anaondoka
Bayern huku akiwa na mataji matatu ya Bundesliga aliyoyavuna katika kila msimu
lakini hakubahatika kuipa ubingwa wa Champions League klabu hiyo ya Ujerumani.
Mara baada ya mchezo huo uliofanyika Allianz Arena na kukabadhiwa rasmi taji
lao, wachezaji wa Bayern Munich wakashangilia kwa staili ya kumtotesha kocha
wao mwili mzima kwa bia.
Guardiola ambaye
kabla hajajiunga na Bayern, alikuwa kocha wa Barcelona, msimu ujao atakuwa bosi
wa Manchester City. David Alaba akimmininia bia kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola baada ya mchezo wa mwisho dhidi
ya Hannover Douglas Costa akiungana na wachezaji wenzake wa Bayern kumwaga
kocha Guardiola kwa staili ya aina yake Guardiola, ambaye msimu ujao atakuwa
kocha wa Manchester City ameshinda mataji matatu ya Bundesliga lakini
ameshindwa kutwaa ubingwa wa Champions League akiwa na Bayern Munich.
0 comments:
Post a Comment