Tuesday, 14 June 2016

EURO 2016:: ITALIA YAILIZA UBELIGIJI ,SWEDEN ,IRELAND HAKUNA MBABE

Italy's Emanuele Giaccherini scores the opening goal past Belgium goalkeeper Thibaut Courtois
Emanuele Giaccherini akiiandikia Italia bao la kwanza ikiwa ni goli lake la kwanza kufunga akiichezea timu ya taifa

ITALIA imeianza vyema michuano ya Euro baada ya kuichapa Ubelgiji magoli 2-0 katika uwanja wa Stade's de Lumiere's katika mchezo wa kwanza wa kundi E.


Emanuele Giaccherin ndiye aliyekuwa wa kwanza kuwafungia Italia goli la kwanza dakika ys 32 baada ya kupokea pasi toka kwa Leornado Bonucci upande wa kulia.

Ubelgiji walikuja juu baada ya goli hilo lakini ukuta wa Italia uliokuwa chini ya Giorgio Chielini, Bonucci na Barzagli ulikuwa makini kuondoa hatari toka kwa kikosi chenye mastaa kibao akiwemo Eden Hazard, Lukaku, Origi pamoja nyota  wengine.

Antonio Conte suffered a nose bleed while celebrating Italy's first goal of the game
Kocha wa Italia Antonio Conte alipatwa na hali ya kuvuja damu puani wakati akishangilia goli la kwanza
Graziano Pelle lashes the ball home in injury time to make sure of the points for Italy
Pelle akiachia shuti lililojaa wavuni na kuiandikia Italia bao la pili
Huku watu wakiamini mchezo huo ungeisha kwa ushindi wa goli moja Graziano Pelle aliipatia goli la pili Italia dakika za nyongeza na kuwafanya  kuibuka na ushindani wa magoli 2-0.
Kevin De Bruyne stretches for the ball with Matteo Darmian also keeping an eye on it 
Kevin De Bruyne akichauana na beki Matteo Darmian (kulia) wakati wa mchezo
Sasa Ubelgiji watalazimika kushinda na kutoa sare michezo miwili iliyosalia ili kujiweka katika nafasi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata.



Italia wanaongoza kundi E wakiwa na alama tatu wakifutiwa na Ireland na Sweden waliotoka sare ya goli 1-1.

Ibrahimovic is congratulated for his part in the leveller by Sweden team-mates John Guidetti and Kim Kallstrom
Nyota wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic akipongezana na wachezaji wenzake, John Guidetti na Kim Kallstrom baada ya timu yao kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Ciaran-Clarkis aliyejifunga katika sare ya 1-1, kufuatia Wes Hoolahan kuanza kuifungia Jamhuri ya Ireland Uwanja wa Stade de France mjini Paris, Ufaransa katika mchezo wa Kundi E Euro 2016


Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA