USAJILI MAJUU:: WIJNALDUM ATUA LIVERPOOL AKITOKEA NEWCASTLE UNITED
Katika kile kinachoonekana kuwa
kocha wa Liverpool inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza ,Klopp kujenga kikosi
kikubwa na tishio ili kurejesha makali ya mabingwa hao wa kihistoria barani
Ulaya, Liverpool imefanikiwa kumnasa mchezaji mahiri na machachari Georginio Wijnaldum toka timu ya Newcastle United kwa ada ya pauni milioni 25 ambapo atavaa jezi namba tano.
Katika siku za karibuni Wijnaldum
alikuwa akihusishwa na vijogoo hao wenye maskani yao jijini Liverpool na
hatimaye tayari amekuwa mmoja wa wanafamilia hiyo.Wijnaldum aliyetua Uingereza
msimu uliopita akitokea PSV Eindhove alijikuta akianza vyema na kuizoea ligi
hiyo mashuhuri na kufanikiwa kuwa mfungaji bora katika timu ya Newcastle kwa
kupachika mabao 11 katika michezo 38.
Katika uhamisho huu inasemekana
licha ya kuwa Newcastle kushuka daraja ndio chanzo, lakini uhusiano kati ya
kocha wa sasa Newcastle Rafa Benitez dhidi ya timu yake ya zamani Liverpool
umekuwa sababu muhimu ya kukamilika.
"Binasfi nina msisimko
kwasababu Liverpool ni klabu kubwa yenye historia kubwa na mara nyingi ni ndoto
ya kila mchezaji kucheza kwenye klabu kubwa kama Liverpool" Wijnaldum aliuambia mtandao wa Liverpoofc.com mara baada
ya kutia saini.
Ni dhahiri kuwa kwa sasa mchezaji
huyu ambaye amekuwa wa sita kusajiliwa msimu huu na anaiongezea Liverpool
uwanja mpana wa uchaguzi katika nafasi za kiungo mshambuliaji na atalazimika
kusafiri kuelekea nchini Marekani ambapo Liverpool imeweka kambi kwa ajili ya
kujiandaa na msimu ujao.
0 comments:
Post a Comment