Monday 4 July 2016

USAJILI::CHELSEA YAKAMILISHA USAJILI WA MICHY BATSHUAYI KUTOKA MARSEILLE

Timu ya Chelsea ya Uingereza imeanza kujiimarisha kwa kufanya usajili wa kwanza wa kumtwaa Michy Batshuayi kwa kitita cha paundi milioni 33 akitokea kwenye klabu ya Marseille kwa mkataba wa miaka mitano.

Mchezaji huyo wa kimataifa raia wa Ubelgiji, alikuwa katika mazoezi hii leo baada ya klabu hizo mbili kukubaliana uhamisho huo mapema wiki hii, wakati Batshuayi akiwa kwenye michuano ya Euro 2016.

Timu nyingine za Uingereza za Crystal Palace na West Ham nazo zilikuwa zinamtolea macho mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, hata hivyo Chelsea ilizizidi kete klabu hizo za Jiji la London.
                         Michy Batshuayi akionyesha jezi yake aliyokabidhiwa na Chelsea

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA