UEFA::BORUSSIA DORTMUND, REAL MADRID HAKUNA MBABE (3-3)
Aliyekuwa mchezaji wa Chelsea Andre Schurrle amefunga goli la kusawazisha la dakika za mwisho wakati Borussia Dortmund ikitokea nyuma na kulazimisha sare ya 2-2 na Real Madrid katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa kundi F.
Real Madrid ilipata goli la kuongoza kupitia Cristiano Ronaldo aliyemalizia mpira wa pasi ya kisigino iliyopigwa na Gareth Bale.
Pierre-Emerick Aubameyang aliisawazishia Dortmund kufuatia kosa la kipa Keylor Navas, lakini baadaye Raphael Varane akaiongezea Real la pili kabla ya Schurrle kusawazisha.
Cristiano Ronaldo akiachia shuti lililoandika goli la kwanza
Mshambualiaji machachari Pierre-Emerick Aubameyang akifunga goli
0 comments:
Post a Comment