EUROPA CUP::GENK YA SAMATTA YAIZAMISHA ATHLETIC BILBAO MABAO 2-0
KRC Genk imeonyesha si timu ya mchezo baada ya kuitwanga Athletic Bilbao ya Hispania kwa mabao 2-0 katika mechi ya Europa Cup.
Genk
iliyokuwa nyumbani, ilipata bao katika kila kipindi huku Mtanzania
akiingia katika kipindi cha pili, ilikuwa dakika ya 56 na kuchangia
kupatikana kwa bao la pili.
Bao
la kwanza lilifungwa na Jakub Brabec aliyeunganisha pasi safi ya Leon
Bailey katika dakika ya 40, wakaenda mapumziko wakiwa wanaongoza.
Samatta aliingia kuchukua nafasi ya Thomas Buffel katika dakika ya 56 na kaanza kuonyesha cheche.
Dakika ya 83, Onyinye Ndindi alifunga bao la pili na kushindilia msumari wa mwisho kwa Wahispania hao.
Bilbao
ni kati ya timu zenye historia ya juu katika La Liga kwa kuwa ni kongwe
na haijawahi kuteremka daraja kutoka La Liga. Nyingine ambazo
hazijawahi kuteremka ni Real Madrid na Barcelona tu.
0 comments:
Post a Comment