GRIEZMANN AFIKISHA MAGOLI HAMSINI LA LIGA, ATLETICO MADRID IKIIBUKA NA USHINDI DHIDI YA VALENCIA
Kipa wa Valencia, Diego Alves ameokoa penati mbili lakini haikusaidia kuizuia Atletico Madrid kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 katika Ligi Kuu ya Hispania.
Antoine Griezmann aliifungia Atletico Madrid goli la kwanza na kisha Kevin Gameiro kuifungia goli la pili.
Kwa matokeo hayo Atletico Madrid inakwea kileleni mwa ligi ikiwa na pointi 15 ilizozipata katika michezo saba.
Mfaransa Antoine Griezmann alifunga goli moja, lakini pia alikosa penati
0 comments:
Post a Comment