SOUTHAMPTON YAIBANA MANCHESTER CITY ,YALAZIMISHA SARE UGENINI
Manchester City imerejea kileleni mwa ligi kuu ya Uingereza licha ya Southampton kusitisha kasi yao ya ushindi kwa kutoka sare tasa.
Wageni Southampton walikuwa wakwanza kufuatia pasi kizembe ya John Stones, kumpa fursa ya kufunga Nathan Redmond aliyemzungusha kipa na kufunga.
City ilianza kuimarika katika kipindi cha pili baada ya kuzomewa na baadhi ya mashabiki wao, na kusawazisha goli kupitia kwa Kelechi Iheanacho aliyetokea benchi.
Nathan Redmond akimzunguka kipa wa Manchester City Bravo
Nathan Redmond akiachia shuti na kufunga goli kwenye goli tu baada ya kumzunguka kipa Bravo
0 comments:
Post a Comment