Thursday 27 January 2022

NAIBU WAZIRI MWAKIBETE AIPONGEZA TCAA KWA UKUSANYAJI WA MAPATO

 

Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete, akisisitiza jambo kwa Mwongoza Ndege Mwandamizi, Bw. Shukuru Nziku, wakati alipotembelea Chuo cha Usafiri wa Tanzania (CATC), jijini Dar es Salaam.



Mkuu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), Aristid Kanje (wa kwanza kulia), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete (wa pili kushoto), kuhusu mipango ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kujenga madarasa, wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya kujenga madarasa hayo jijini Dar es Salaam. 


Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete, akisisitiza jambo kwa wanafunzi wanaosoma Chuo cha Usafiri wa Tanzania (CATC), jijini Dar es Salaam.

Mkurungenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Hamza Johari akitoa maelezo juu ya uendeshaji wa mamlaka hiyo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi (Uchukuzi) Atupele Mwakibete mara baada kutembelea Makao Makuu ili kujifunza ufanyaji kazi wake

Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete (wa tatu kulia), katika picha ya pamoja na Menejimenti  ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzanai (TCAA), mara baada ya kutembelea Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam. 



Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete, ameipongeza Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzanai (TCAA), kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato kupitia Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC), ambapo katika mwaka huu wa fedha 2020/21  kimeweza kukusanya takribani Shilingi Bilioni 2 kutoka Milioni 500 zilizokusanywa 2017/2018 na hivyo kuongeza mapato ya Mamlaka kufikia zaidi ya Bilioni 45 kwa mwaka.

Ameongeza kuwa makusanyo hayo yametokana na uwepo wa miundombinu bora ya chuo  hicho kuwa ya kisasa ikiwemo mifumo ya kisasa ya mafunzo kwa vitendo (Simulator) za kufundishia kozi mbalimbali chuoni hapo.

Akizungumza hayo jijini Dar es Salaam, wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea Mamlaka hiyo na chuo hicho ambapo pamoja na mambo mengine ameipongeza TCAA kwa kuweka mikakati thabiti katika uthibiti katika usafiri wa anga na kuitaka mamlaka kuendelea kuwekeza katika wataalam ili kukidhi mahitaji ya udhibiti.

“Nakupongeza sana Mkurugenzi Mkuu kwa kuweka mikakati mizuri ya mwendelezo wa taasisi yako, nimefarijika sana kusikia mna miradi ambayo mnaitekeleza kwa kutumia fedha zenu wenyewe kama mradi ya rada nne, hili ni la kupongeza”, amesisitiza Naibu Waziri Atupele.

Akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Bw. Hamza Johari, amesema pamoja na ongezeko la mapato ya Mamlaka iko kwenye hatua mbalimbali ya kujenga majengo ya kisasa ambayo yatarahisisha utoaji wa elimu chuoni hapo.

“Idadi ya wanafunzi tunaopokea imekuwa ikiongezeka na kama ulivyoona tuna madarasa machache sana, ila mipango iliyopo kwa sasa ni hukakikisha tunajenga majengo kwenye eneo uliliona ili wanafunzi wetu wasome kwenye mazingira rafiki", amesema Bw. Johari.

Vilevile Mkurugenzi Mkuu amesema pamoja na kuimarisha chuo hicho ambacho kimekuwa sehemu ya pato kwa Mamlaka, mipango mingine iliyowekwa katika kuboresha utendaji ni kuongeza wataalam kwenye fani mbalimbali ili kwenda sambamba na maboresho yanayofanywa na Serikali kuboresha usafiri wa anga.

Naibu Waziri Atupele yuko mkoani Dar es Salaam kwa ajili ya kutembelea, kufahamiana na kuzungumza na viongozi na watumishi waliopo katika taasisi za Sekta ya Uchukuzi na pamoja na kukagua miradi ya kisekta. 

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikali, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA