MATUKIO KATIKA PICHA KUHUSU AJALI YA NDEGE ILIYOUWA WACHEZAJI WA BRAZIL
Mabaki ya ndege namba CP 2933 iliyoanguka katika jimbo la Medellin nchini Colombia huku ikisemekana kuwa watu 75 wamepoteza maisha wakiwemo wachezaji wa timu ya Chapecoense ya nchini Brazil
Kikosi cha waokoaji kikiendelea na zoezi la kutoa miili ya watu walioaga dunia katika ajali hiyo
Mashabiki wa Chapecoense wakiwa wamejikusanya kwenye makao makuu ya klabu hiyo maeneo ya Chapeco nchini Brazil
Waokoaji wakiwa wamebeba moja ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo
Shughuli za uokoaji zikiwa zinaendelea huku taarifa zikisema ni watu sita pekee ndio waliotoka wakiwa hai
Waokoaji wakipanga miili ya baadhi ya abiria waliofariki
Hii ndio ndege iliyopata ajali
Mchoro ukionyesha safari ya ndege hiyo kabla haijapata ajali
Mchezaji Jackson Follmann ametajwa kuwa ni kati ya watu sita walionusurika katika ajali hiyo
Kikosi cha Chapecoense
Hapa viongozi na wachezaji wa timu hiyo wakiwa ndani ya ndege kabla hawajaanza safari iliyokatisha uhai wao
Beki wa timu hiyo Alan Rushel aliposti video kwenye mtandao wa Instagram akiwa na kipa Danilo kabla ndege haijaondoka nchini Brazil
Rushel alikuwa wa kwanza kukimbizwa hospitali kupata matibabu huku akiwaasa madaktari kuwa makini na pete yake ya ndoa isijepotea
Kikosi cha huduma ya kwanza kikiwa jirani na eneo la tukio
Meya wa jiji la Medellin, Fico Gutierrez akiwasili katika eneo la tukio
Madaktari na wauguzi wakisubiri majeruhi ili kuwahudumia
Rushel na Danilo wanatajwa kuwa ni kati ya abiria sita waliotoka wakiwa hai
Nembo ya klabu hiyo iliyookotwa baada ya ajali hiyo
Ndege hiyo iligawanyika vipande viwili baada ya kuanguka
Madaktari wakijitahidi kuokoa uhai wa mmoja wa abiria wa ndege hiyo
Simanzi kubwa.....wachezaji watatu ambao hawakusafiri na timu wakiwa na huzuni kubwa ndani ya chumba cha kubadilishia nguo cha timu hiyo
Ndugu, jamaa na marafiki wakisubiri taarifa kutoka eneo ilikotokea ajali
0 comments:
Post a Comment