Wednesday 30 November 2016

MATUKIO KATIKA PICHA KUHUSU AJALI YA NDEGE ILIYOUWA WACHEZAJI WA BRAZIL

Mabaki ya ndege namba CP 2933 iliyoanguka katika jimbo la Medellin nchini Colombia huku ikisemekana kuwa watu 75 wamepoteza maisha wakiwemo wachezaji wa timu ya Chapecoense ya nchini Brazil


 Kikosi cha waokoaji kikiendelea na zoezi la kutoa miili ya watu walioaga dunia katika ajali hiyo


 Mashabiki wa Chapecoense wakiwa wamejikusanya kwenye makao makuu ya klabu hiyo maeneo ya Chapeco nchini Brazil


 Waokoaji wakiwa wamebeba moja ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo


Shughuli za uokoaji zikiwa zinaendelea huku taarifa zikisema ni watu sita pekee ndio waliotoka wakiwa hai


 Waokoaji wakipanga miili ya baadhi ya abiria waliofariki 


 Hii ndio ndege iliyopata ajali


 Mchoro ukionyesha safari ya ndege hiyo kabla haijapata ajali 


 Mchezaji Jackson Follmann ametajwa kuwa ni kati ya watu sita walionusurika katika ajali hiyo


 Kikosi cha Chapecoense


 Hapa viongozi na wachezaji wa timu hiyo wakiwa ndani ya ndege kabla hawajaanza safari iliyokatisha uhai wao


Beki wa timu hiyo Alan Rushel aliposti video kwenye mtandao wa Instagram akiwa na kipa Danilo kabla ndege haijaondoka nchini Brazil


 Rushel alikuwa wa kwanza kukimbizwa hospitali kupata matibabu huku akiwaasa madaktari kuwa makini na pete yake ya ndoa isijepotea


 Kikosi cha huduma ya kwanza kikiwa jirani na eneo la tukio


 Meya wa jiji la Medellin, Fico Gutierrez akiwasili katika eneo la tukio


Madaktari na wauguzi wakisubiri majeruhi ili kuwahudumia


Rushel na Danilo wanatajwa kuwa ni kati ya abiria sita waliotoka wakiwa hai


 Nembo ya klabu hiyo iliyookotwa baada ya ajali hiyo


 Ndege hiyo iligawanyika vipande viwili baada ya kuanguka


 Madaktari wakijitahidi kuokoa uhai wa mmoja wa abiria wa ndege hiyo





Simanzi kubwa.....wachezaji watatu ambao hawakusafiri na timu wakiwa na huzuni kubwa ndani ya chumba cha kubadilishia nguo cha timu hiyo


Ndugu, jamaa na marafiki wakisubiri taarifa kutoka eneo ilikotokea ajali

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA