Tuesday 28 June 2016

USAJILI::LIVERPOOL YAKAMILISHA UHAMISHO WA SADIO MANE


Timu ya Liverpool imekamilisha kunasa saini ya raia wa Senegal Sadio Mane, 24, kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 34 kutoka Southampton.

Mane anajiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka mitano, ikiwa ni mchezaji wa tatu kusaini na Liverpool katika majira ya joto baada ya kipa Mjerumani Loris Karius pamoja beki wa Mcameroon, Joel Matip.

Dau la nyota huyo wa Senegal ada yake itaongezeka na kufikia paundi milioni 36, na kuweza kumudu kupiku rekodi ya paundi milioni 35 ya Andy Carroll mwaka 2011 wakati alipokuwa mchezaji ghali kujiunga na Liverpool.
                                     Sadio Mane akisaini mkataba wa kujiunga na Liverpool 
                Sadio Mane akionyesha jezi aliyokabidhiwa katika timu ya Liverpool


0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA